Nedy Music Atamani Kufanya Kazi na Alikiba na WCB

Msanii wa Bongo fleva Nedy Music anayefanya vizuri hivi sasa na wimbo wake wa One and only amefungukia mipango yake ya kufanya Kolabo na staa wa Bongo fleva Alikiba Lakini pia kusainiwa WCB.

Nedy Music anayefanya muziki wake chini ya label ya PKP ya msanii Ommy Dimpoz amefunguka na kuweka wazi kuwa endapo itatokea nafasi ya yeye kusainiwa WCB basi ataichukua kwani ni uamuzi wa kibiashara:

download latest music    

Nedy Music amefungukia  kusaini katika label ya WCB amesema ikitokea nafasi hiyo atasaini kwa sababu ni biashara, pia amekanusha taaarifa za kuachana na label yake ya PKP mara baada ya wimbo wake mpya kutoka bila kuwa na logo ya label hiyo.

Kwenye Interview aliyofanya na The Playlist ya Times Fm, Nedy Music aliweka wazi kuwa yupo tayari kufanya kazi na Ali Kiba lakini anataka afanye naye kazi huku watu waone amestahili kufanya naye kazi kwa ajili ya kipaji chake alichonacho na sio sababu anamfahamu tu Kiba basi ndio afanye naye Kolabo:

Unajua usifanye kitu kimazoea, usifanye kitu kwakuwa unajuana na mtu nilitamani watu wajue uwezo wangu, nikiwa na maana hata pale ninapoenda na kazi nataka afanye na mimi basi pawe na urahisi na si kinyonge atafanya kwa kuwa tunajuana, kwa hiyo ni wazo bado lipo na panapo majaliwa litatokea”

.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.