Nedy Muziki Awaumbua Washkaji Wanaomsumbua Mpenzi Wake.
Msanii anaetamba na kibao chake cha one and aonly alichomshirikisha Ruby amefunguka na kuwarushia madongo baadhi ya washkaji zake ambao wamekuwa wakimsumbua mwanamke wake kwa kumtongoza na kusema kuwa anaawajua kwa sababu anaona meseji zote ambazo zinakuwa zinaingia katika simu ya mpenzi wake huyo.
Akiandika hayo katika ukurasa wake wa instagram akiwa ameweka picha yake na mpenzi wake huyo Nedy muziki anasema kuwa anawajua watu wote alionao karibu ambao wamekuwa wakimfanyia majungu kwa mpenzi wake huyo na hata wale ambao wamekuwa wakimtongoza shemeji yao na screen shots anazo hivyo anawasubiri kuwaumbua na wala haogopi kufanya hivyo.
Kama nawaona washkaji zangu wanafiki wanavyohaha muda huu kujiuliza files zao na amdishi yao ya kishamba yoote nnayo, screenshots, txt za majungu na kujitongozesha zaidi kweli washkaji zangu ku…..nyoko #mpemba haachimpakakufa #jiandaekufichasurayakokwaaibu.
Imekuwa ni kama tabia kwa wasanii kuwa wanatafuta kiki ywa kutangaza kuwa wasanii na washkaji zao wamekuwa wakiingilia mahusiano yao au kuwatongoza wanawake zao , na baada ya hapo kiki hiyo inaweza kuja kuzimwa kwa kuachia wimbo mpya, haijajulikana kwa Nedy amekuwa akimlenga nani.