Ney wa mitego Alitumwa na Clouds Atuimbe Mimi na P-Funk:-Dudu Baya

Mwanamuziki Dudubaya amefunguka na kusema kuwa anajua figisu zilizokuwepo kati yake na Clouds mpaka kufikia hatua ya kumtuma Nay wa mitego ili atunge wimbo  na kuwimba wasanii amba walikuwa hawana nguvu kipindi icho bila kuua kuwa kuna watu wanapanda na kushuka hivyo hakuna anaejua kesho yake.

Akiongelea muziki wa Nay wa mitego kwa sasa , Dudu Baya anasema kuwa Nay wa mitego kwa sasa amegombana na T-touch na tangu walipogombana na Producer huyo hakuna nyimbo yake hata moja ambayo inafanya vizuri kwa sasa .

download latest music    

Hata hivyo dudu baya anasema kuwa msanii huyo ambae amekuwa akiimba nyimbo za kuakosoa baadhi ya wasanii  aliwahi kutumwa na Clouds media kwa ajili ya kuwaimba wao ambao walikuwa wamushuka kimuziki kipindi hicho.

Anasema “Unamuona msanii kama nay wa mitego amekuwa aisema kuwa wasanii wa wasafi hawana amsha amsha , hivi ana akili timamu kweli, msanii huyo  alitumwa na Clouds kuandika wimbo wa amepanda ameshuka ili kutuimba mimi na p-funk, anawatukana ma-legendary walioiza bongo fleva.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.