Ney wa Mitego Amefunguka Baada Kumtabiria Diamond Kushuka Kimuziki

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kurap Ney wa Mitego amefunguka na kuongelea jambo ambalo lilimfanya atengeneze headlines kwenye mitandao ya kijamii siku za nyuma kidogo kuhusu Diamond kushuka kimuziki.

Ney wa Mitego alishangaza watu wengi alipoanza kumponda Diamond ukitegemea wamekuwa marafiki kwa kipindi kirefu na hata wamefanya mziki kwa pamoja ambapo amemshirikisha kwenye nyimbo yake iliyofanya vizuri sana miaka ya nyuma ‘Muziki gani’.

download latest music    

Hivi karibuni kupitia mtandao wa Instagram, Ney aliweka picha ya mnyama simba akionekana akiuwawa kikatili jambo lilitafsiriwa kuwa yule ni Diamond kutokana na tayari inajulikana jina jingine la Diamond ni Simba akimaanisha yeye ni mfalme wa mwituni.

Kwa kuweka picha ya Simba akiuwawa ilisemekana kuwa au ilitfsiriwa kuwa Ney wa Mitego alikuwa anatabiri Diamond kushuka kimuziki. Kwenye mahojiano aliyofanya Times Fm katika kipindi cha The playlist Ney amesema hakukusudia jambo lolote baya ama hakua na nia mbaya dhidi ya Diamond kwa sababu ni mshkaji wake.

Diamond ni mshkaji wangu tumefanya kazi kubwa sidhani kama imefika hatua ya sisi kuwa maadui kiasi hicho na siwezi kumuombea mabaya kiasi hicho lakini tunaona changamoto anazopitia. Nilijua tu ile picha wabongo kila mmoja ataongea la kwake lakini sina tatizo na Diamond lakini hata kama lipo basi tutalimaliza lakini ile picha ilikuwa haimuhusu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.