Ney Wa Mitego Athibitisha Hakuna Ugomvi Kati ya Godzilla na Billnass

                                                     

 

download latest music    

Msanii wa bongo fleva anaetamba na kibao chake cha makuzi ney wa mitego amesema kuwa hakuna ugomvi wowote kati ya msanii Godzilla na Billnass kama watu wanavyosema katika mitandao, Ney wa Mitego amesema hayo baada ya kuwakutanisha wasanii hao wawili na kuweza kufanya nao kazi moja ambayo  inajulikana kama  muda wetu Remix ambayo pia ameshirikishwa AY.

Katika mitandao na baadhi ya vyombo vya habari kulikuwa na maneno kuwa billnass amekuwa akiiga nyayo za godzilla na kwamba kutokana na hayo wawili hao wamekuwa na bifu la kimuziki kutokana na maslahi ya musiki huo.

Akiongea katika Radio One , Nay wa Mitego amesema kuwa wsanii hao wawili hawana tofauti yoyote kama watu  wanavyosema kuwa wamekuwa na tofauti ya muda mrefu na kwamba nafasi ya Godzilla amezibwa na billnass katika game.

Mdundo ulinifanya nimuone Godzilla lakini pia mdundo ulinifanya nimuone  pia Billnass, licha ya kuwa kumekuwa na maneno katika mitando kuwa wili hao wamekuwa na tofauti ya muda mrefu lakini watu hao hawana tofauti yoyote.-Alifunguka Ney Wa Mitego.

Hata hivyo ney wa mitego aliongezea na kusema kuwa watu wengi katika mitandao wamekuwa na tabia ya kuvuruga maneno na kuzusha vitu vya uongo bila kujua ukweli wa kila kitu.

Naweza kusema kuwa mitandao au maneno ya watu yanaweza kuchochea kitu  na watu wakafanya kukawa na ugomvi, na ugomvi ukawa mkubwa wakati watu  wanakuwa hawana tofauti yoyote.-Alimazia Ney wa Mitego

 

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.