Ni matatizo ya Kifamilia Yaliyoniachanisha na Aslay-Tessy
Mwanadada Tessy Chocolate amefunguka na kuelezea kwa nini ameachana na baba wa mtoto wake aslya ambae ni msanii wa bongo fleva naefanya vizuri sana katika anga hizo.
Akiongea na moja ya waandishi wa habari kutoka Ayo Tv, Tessy anasema kuwa kuachana kwake na Aslay ni mambo ya kawaida tu ya kifamilia ambayo yanaweza kutokea kwa mtu yoyote katika ndoa .
Hatuko pamoja tena na hayo ni matatizo tu ya kifamilia ambayo nadhani yanaweza kutokiea kwa kila mtu, au kila mtu anaweza kuyapitia ila ni ya kawaida tu ya kifamilia.
Hata hivyo Tessy alipoulizwa kwanini hakuwa wazi tangu hapo awali kuhusu kuvunjika kwa mahusiano yao, alijibu kuwa amekuwa hapenzi sana maisha yake yakae katika mitandao ya kijamii.
Hakuna aliyewahi kunikataza kuongelea kuachana kwetu lakini ninasema tena sipendi mahusiano yangu yakae katika mitandao ya kijamii, kwa sababu hayo ni maisha yangu binafsi.