“Nikifa Leo Mwanangu Asinizike Wala Asiguse Jeneza Langu”- Baba Diamond

Baba mzazi wa msanii wa Bongo fleva, Diamond Platnumz pamoja na dada yake staa mkongwe wa Bongo fleva anayejulikana kama Mzee Abdul Juma, ameibuka na kudai kuwa endapo akifa hata leo kesho basi mtoto wake asimzike wala asiguse jeneza lake.

Baba Diamond amekuwa hana uhusiano mzuri na watoto wake wote wawili yaani Diamond na Queen Darlene mara kwa mara amekuwa akuongea na vyombo vya habari kuhusuatatizo aliyonayo kwenye familia yake.

download latest music    

Hivi karibuni Queen Darlene alifanya mahojiano na kituo kimoja na katika maongezi yake kuhusu wifi yake Zari, alimuingiza baba yake mzazi Mzee Abdul ambapo alisema:

Zari ni wifi mzuri kwangu ana roho nzuri na ndiye mtu pekee aliyekuwa ananishauri kumjali baba yangu, japo baba mwenyewe kuumwa kwake kumekuwa kama mtoto kwa kweli kwa sasa siwezi kusema baba yangu ni Abdul baba yangu ni Naseeb”.

Baada ya mzee Abdul kusikia kuhusiana na maneno aliyoongea binti yake alikasirishwa na kumwambia kuwa endapo akifa basi Queen Darlene asiguse jeneza lake wala hata asithubutu kumzika kwenye mahojiano na Global TV alifunguka yafuatayo:

Nimeumia sana kwani Queen Darlene yeye ni nani hata kunyanyuka na kusema maneno kama hayo kanichukulia mimi kama mtoto hata kama ni dharau sio hivyo kaka yake mwenyewe ambaye ametoka kimuziki na anafanya vizuri hata kama ananidharau hajawahi kunitamkia maneno kama hayo iweje leo hii Queen Darlene anitamkie maneno kama haya Queen Darlene ni binti yangu ambaye nimekaa naye kwa muda mrefu sana na mara nyingi amekuwa akija hapa nyumbani tunapika tunakula lakini leo hii inakuaje baada ya kutoka kimuziki anaanza kutoka kimuziki anaanza kunidharau mimi nimeumia sana sasa na mimi niseme nikifa hata leo na yeye asije kabisa assogelee jeneza langu wala asinizike yeye si kasema baba yake Naseeb basi na mimi sio baba yake “.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.