Nikki Mbishi Amjibu Dudubaya Kuwatetea Chege na Madee.
Siku chache zilizopita , msanii Dudubaya alitoa mapovu kuhusu wimbo wa madee na chege na kuwaambia kuwa wamekuwa wakifanya kazi zao huku wakijikita sana katika maazi ya kiafrika ya kusini kuliko ya kitanzania .Imekuwa kawaida kwa msanii Dudubaya kuwa akiponda nyimbo za wasanii wengine na kusema kuwa hawajui kufanya kazi za muziki.
Sasa basi amneno hayo yamemgusa , nikki mbishi na hivyo ameamua kumjibu Dudubaya kwa kile alichokisema kuhusu Madee na Chege na kumwambia kuwa kama anaona wenzake wamekuwa wakikosea basi anatakiwa kutoa mfano wa hivyo vitu vizuri ili wasanii wengne wamuige na sio kukaa anaponda bila yeye kufanya kitu chochote.
unajua saa zingine kukaa unaongelea miziki ya watu wengine wakati wewe mwenyewe haujatoa kitu ambacho kiko perfect tukisikie, tuonyeshe basi mamba, dudabaya kwamba jiwe langu hili hapa sijaiga south wala wapi nyie mnaonaje, maana mimi ninaamini sana kwenye kutoa kazi kuliko kukaa kimya na kukosoa.