Nikki Mbishi- Watangazaji Acheni Kuuliza Maswali ya Diamond na Ali Kiba

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nikki Mbishi amefunguka kuhusu kuchoshwa na Watangazaji wa vyombo vya habari ambao wamekazania maswali ya Diamond na Ali Kiba.

Diamond na Ali Kiba ni wasanii wakubwa kabisa wa Bongo fleva Lakini pia bifu walilonalo limekuwa likileta mgawanyo baina ya wasanii mbali mbali.

download latest music    

Hivyo ni swali la kawaida kwa wasanii kuulizwa kama wanapenda muziki wa Diamond au Ali Kiba lakini swali hilo limeonekana lumkera Nikki Mbishi ambaye amemwaga povu zito.

Nikki Mbishi amesema katika interview maswali kuhusu Diamond na Alikiba ndio hushamiri ila anachojivunia ni kwamba na yeye uhoji pia.

Kwenye m ukurasa wake wa twitter Nikki Mbishi amefunguka haya:

Kila interview wanauliza “Una mpango wowote wa kufanya ngoma na Ali Kiba au Diamond?” Hapo basi mtangazaji ndio anajiona kamaliza mwenyewe…#UFALA

Wakiitwa wengine interviews wanahojiwa ila nikiitwa mimi nawahoji wao ndio maana wanakuwa mabubu nikitimba….I’m proud of it. Great monday to all pointless and dumb presenters out there,peace!”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.