Nikki Wa Pili Aandika Barua Ya Kumlilia Ruge

Msanii wa muziki wa Hip hop nchini Nickson Simon maarufu kama ‘Nikki wa pili’ amefunguka na kuweka wazi barua aliyomuandikia Mkurugenzi wa Clouds Media Ruge Mutahaba.

Siku chache zilizopita familia ya Clouds Media iliweka wazi kuwa Ruge yupo hoi hospitalini kutokana na maradhi ambayo yamekuwa yakimuandama kwa kipindi kirefu sasa.

download latest music    

Msanii Nikki wa Pili amefunguka mengi kuhusu Ruge na hata kutaja mambo mengine mengi ambayo amemfanyia ambayo mpaka leo yameweza kumpa mafanikio makubwa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nikki wa Pili aliandika maneno haya:

Muda wa kipindi kirefu sana katika maisha yangu ya shule nilikuwa naamini mim ni mtu wa kukaa nyuma, nisiye na uwezo wa kuzungumza mbele za watu, sikuwa nanyoosha mkono darasani hata kama najua jibu, nilio soma nao chuo wanajua nilivyo kuwa natoroka presentations.

Muda wa kipindi kirefu sana katika maisha yangu ya shule nilikuwa naamini mim ni mtu wa kukaa nyuma, nisiye na uwezo wa kuzungumza mbele za watu, sikuwa nanyoosha mkono darasani hata kama najua jibu, nilio soma nao chuo wanajua nilivyo kuwa natoroka presentations.

Akaniambia wewe ni public speaker mzuri, akaanza kunipa nafasi ya kuzungumza mbele za watu nilikuwa naona na kosea lakini kila niliposhuka alikuwa anaiambia umefanya vizuri sana ongeza hichi na hichi.

Leo nimekuwa naalikwa vyuoni, kwenye makongamano, semina,taasisi, kampeni mpaka makanisani, kama mzungumzaji au mtoa mada, na hata mitandaoni huwa naandika mawazo yangu bila woga, ingekuwaje nisingekutana na Ruge Mutahaba.

Mungu akupe wepesi urudi katika uzima wako, RG (genius)”.

Inaripotiwa Ruge yupo nchini Afrika Kusini akipatiwa matibabu kutokana na matatizo ya figo ambayo yanamsumbua kwa miezi kadhaa sasa.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.