Nikki wa Pili Amjibu Mh.Nasarri Kuhusu Mh. Sugu

Msanii wa muziki nchini Nikki wa Pili amemjibu Mh Joshua Nassari baada ya kuwatuhumu wasanii kwa kukaa kwao kimya baada ya Mh.Sugu kukamatwa na kuweka polisi kwa zaidi ya siku kumi sasa wao wakiwa wamekaa kimya ilhali mbunge huyo alikuwa mstari wa mbele kuwatetea wasanii katika kupata maslahi yao.

Mh. Nasari anawataka wasanii wakumbuke kuwa Sugu ndie msanii wa kwanza kupigania haki zao kwa uda mrefu na kukataa kufanya kazi za muziki  bila kulipwa na haki hiyo.

download latest music    

wasanii wa bongo fleva mmesahau kabisa harakati za sugu kupigania muziki wenu kusimama.sugu yupo selo siku ya kumi sasa wasanii mmepiha kimya,courtin hamtokei,jela hamji kumuona , mmeamua kumtumikia kafiri.mmesahau kuwa alianzisha harakati za kugoma kuimba bure.

Katika kumjib Mh. Nassari nikki wa pili amemwambia kuwa wasanii wanaogopa kupaza sauti ya kutetea jambo kwa sababu hakuna umoja kati yao na hata wanapotaka kusimama kutetea jambo fulani mtu anaweza kujikuta peke yake.

Wasanii hawna umoja na chama chao hakina nguvu kwaio hata kinapotokea kitu  wasanii wakatakiwa kulitolea sauti hakuna platform   ya kulishikilia jambo hilo  na kujikuta kila msanii huyo yuko peke yake  na kupaza sauti peke yae wasanii wengi wanaogopa hilo.-Aliandika Nikkki wa Pili.

Mheshimiwa joseph mbilinyi jina la usanii sugu aliwekwa jela siku kama 10 zilizopita kwa tuhuma za kutoa maneno ya uchochezi kwa wananchi juu ya serikali iliyopo madarakani.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.