Nikki Wa Pili Atangaza Ndoto Yake ya kuwa Raisi, Wasanii Wamsapoti.
Akiwa kama moja ya wasanii wanaojitahidi sana kutoa maneno yenye kuhamasisha katika jamii,nikki wa pili kwa mara ya kwanza ameweka wazi kuwa ndoto yake kubwa ni kuwa rais, ingawa msanii huyo kwa sasa hajaweka wazi kuwa yeye ni mfuasi wa chama gani lakini amekuwa akihamasiha sana vijana kupitia mitandao ya kijamii.
katika ukurasa wake wa twitter, Niki wa Pili aliandika”Ndoto yangu ni kuja kuwa Rais”
Hata baada ya kuweka tweet hiyo , baadhi ya wasanii walionekana kumsapoti msanii huyo kwa kumpongeza kwa kuwa na ndoto hiyo huku wakimtaka asikate tamaa,mmoja kati ya wasanii hao ni Dogo Janja ambae aliandika
ndoto yako ipalilie tu ndugu yangu, anayeona haliwezekani hilo ni tatizo lake sio kwako, husda ni tunu ya Taifa, isikusumbue fanya mambo yako #Nikiwapiliforthepresidency