Nikki wa Pili Awatolea Uvivu BASATA.

Ikiwa bado sakata la kufungiwa kwa wasanii likiwa bado linashika kasi katika mitandao ya kijamii huku wengi wao wakingngunika kwa jinsi msanii wa bongo hip -hop ,Roma Katoliki alivyopewa adhabu kubwa ilhali muda wake wa kufanya marekebisho ya nyimbo hiyo yakiwa bado haujaisha msanii ,mwenzake Nikki wa Pili kutoka kundi la Weusi ameilalamikia BASATA kuhusu hatua kali wanazochukua wa wasanii huku akiwakumbusha mambo ya nyuma yaliyopita hasa kipindi cha siasa jinsi kulivyokuwa kumetapakaa kwa nyimbo za matusi lakini zilikuwa hazifanywi kitu chochote..

Niki wa Pili ambae amekuwa msemaji mzuri katika kitandao ya kijamii kuhusu maswala mbalimbali yanayotokea katika jamii anasema kuwa imekuwa  basata wamekuwa wakifumbia macho baadhi ya vitu na kuibuka na baadhi ya vitu kitu kinachowafanya watu waone kama vile hawatendi haki.

download latest music    

Akihoji kuhusu maamuzi ya BASATA , Niki  wa Pili amehoji kwanini kipindi cha kampeni kulikuwa na nyimbo nyingi za siasa zilizokuwa na matusi mengi lakini hazikuwa zikifungiwa lakini wameanza kuwakamta wasanii wenzao.

tukizungumzia nyimbo za matusi bwana zilizotoka wakati wa kampeni , bwana we matuzi ya nguoni,tena takitukana watu wazima  na heshima zao,hapa walezi wetu wakikaa kimya bBASATA kama walezi  wetu msisahau kuwa kuyalinda maadili yetu kiuchumi , kama mlezi  halafu watoto wako wanakuwa wanaishia kufa , inamaanisha hawakulelewa vizuri kiuchumi pia-Aliandika Niki wa  Pili akitaka BASATA kwaangalia pia wasani wake katika swala la kiuchumi.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.