Nikki Wa Pili- Sitafuti Kiki Ni Ndoto Yangu Kugombea Uraisi

Msanii wa muziki wa hip hop nchini kutokea katika kundi la Weusi, Nickson Samson maarufu kama Nikki wa Pili amefungukia mipango yake ya Kugombea uraisi mwaka 2025.

Wiki iliyopita Nikki wa Pili alitrend Kwenye mitandao ya kijamii kwa taarifa ya kwamba ana mipango ya kugombea uraisi na hata kuna mashabiki walimtuhumu kwa kutafuta kiki Kupitia ishu hiyo.

download latest music    

Kwenye mahojiano na gazeti la Risasi Vibes, Nikki wa Pili alianika kwamba siyo kiki bali ni kweli ana mpango wa kuwania Urais wa Tanzania.

Watu wanaweza kufikiri kwamba ninatafuta kiki, lakini ukweli ni kwamba ni ndoto yangu siku moja kuwa Rais wa Tanzania. Kwa sasa ninasogeza umri, baada ya mwaka 2025, nitafahamu ni chama gani kitanipa tiketi.

Kuhusu nafasi hii ‘CV’ yangu inajieleza na namna ambavyo watu wananiamini, nitaendelea kufanya mambo ya kujenga uaminifu zaidi ili baadaye niwatumikie Watanzania”.

Siku za nyuma mbunge wa Kigoma Mh. Zitto Kabwe alishawahi kumtaka Nikki Wa Pili ajiunge na ACT Wazalendo Kupitia ukurasa wa Twitter jambo ambalo Nikki alikataa na kusema yeye sio mwanasiasa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.