Niliaka Kulia Baada ya Kusikia Q-Chillah Anaacha Muziki-T.I.D
Msanii T.I.D ameonga kwa kumdharau msaniimwenzake Q-chillah na kusema kuwa aliposikia msanii mwenzie huyo anataka kuacha muziki alitaka kulia maana alijua kabisa kuwa ni uongo na alikuwa anatafuta namna ya kutoka katika muziki wake unaokuja.
Akiongea katika radio moja alipokuwa akifanyiwa mahojiano , T.I.D alipoulizwa kuhusu alijisikiaje aliposikia msanii Q-C hilah anaacha muziki, msanii huyo alijibu huku akicheka
” nilitaka kulia kwa sababu nilijua kabisa kuwa hiyo ilikuwa ni katoro, nilijua kabisa kuwa yule alikuwa akitufunga kamba, hasa zile ndo kiki, mtu anatafuta kiki hasa .
Miezi kadha hapo nyuma msanii Q-chief alitangaza kuwa anacha muziki kutokana na matatizo mbalimbali yanayomkabili hivyo aliona kuwa bora ajiengua katika sanaa hiyo, lakini baadae alikuja kusema kuwa amepkea moni mengi na aliona kuwa bado watu wanamuhitaji katika muziki hivyo alitaka kurudi kwa ajili yamashabiki na baada ya hapo aliachia ngoma yake mpya.
Hata baada ya kutoa ngoma yake , wengi walimuhukumu na kusema kuwa kutangaza kwake kuacha muziki ni kiki tu na wala haikuwa kweli.