“Nilikuwa nakunywa pombe sana” Saida Karoli

Kama wasanii wengi Saida Karoli ambaye ni muimbaji na pia mama hivi karibuni alifunguka kueleza baadhi ya vitu ambazo zilimfanya kuteleza kutoka kwa muziki akizungumza kwenye mahojiano na Clouds FM.

Saida ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya wa ‘Orugambo’, alisema kuwa alijipata ameanza kutumia pombe lakini baada ya kugundua kuwa haikuwa na faida basi aliwacha na tangu 2006 hajagusa ata bia… Saida alisema,

download latest music    

“Vitu vingi nilipitia ila namshukuru Mwenyenzi Mungu sikufikia hatua ya kusema najiuza, na mpaka mtu anafikia anaona yeye sio kitu anaenda kujiuza barabarani, kuuza mwili wake lakini mimi sikufanya hivyo,”

Msanii huyu aliendelea kusema,

“Nilikuwa nakunywa pombe sana lakini kutokana na kushuka kwangu nikaona na pombe niache tangu mwaka 2006, situmii bia, situmii Sigara namshukuru Mwenyenzi Mungu amenipa ustahimilivu nimesimama wima hatimae nimerudi Saida yule yule.”

Hata hivyo kwa sasa amejiandaa kuwachia album yake hivi karibuni.

 

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua