Nilipiga Stop Kitendo Cha Wema Kuwepo Kwenye Video Ya Roma-Mke Wa Roma

Wasanii wa hip hop wanaounda kundi la Rostam Roma Mkatoliki na Stamina wameachia kazi yao mpya “Kaolewa” ambayo mpaka sasa inafanya vizuri kwa hewa.

Kwenye video hiyo yupo msanii wa Bongo movie Nisha ambaye amecheza uhusika wa Mwajuma lakini inadaiwa uhusika huo alitakiwa acheze Wema Sepetu lakini Mke wa Roma alikataza kitendo hiko.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Mke wa Roma amefunguka na kuweka wazi kuwa alimkataza mume wake kumtumia Wema Sepetu kwa sababu aliamini Nisha angefanya kazi nzuri zaidi na kuvaa uhusika:

Wakati wanaenda kushoot video nililetewa option ya video Queen wenyewe walikuwa wanataka kumchukua Wema Sepetu nikawaambia Hapana Wema hayupo Kwenye uhusika wa hiyo nyimbo yenu nikawaambia kama mnataka Msanii atakayevaa uhusika vyema basi mchukueni Nisha, na kweli Nisha amevaa uhusika vizuri sana na video imependeza”.

Wema Sepetu ameshawahi kuonekana kwenye video ya wimbo wa Diamond tu na alishawahi kusema hawezi kufanya video za wasanii wengi.

Video ya wimbo wa Rostam ‘Kaolewa’ inaendelea kufanya vyema na sasa inashika chati kwa kutrend namba 3.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.