“Nilishalala njaa sana tu” Snura Mushi afunguka kuhusu maisha yake ya tabu

Ukiona vyaelea vimeundwa… Snura Mushi ametoka mbali kufika alipo sasa. Mwimbaji huyo amepitia yote ya maisha ikiwemo kulala njaa.

Snura amekana dhana iliyojengeka kwa akili ya watu wengi kuwa kila mwanamke mwenye mafanikio ya aina yoyote lazima atakuwa ameyapata kutoka kwa wanaume aliotembea nao kimapenzi.

download latest music    

Mwimbaji huyo amesema kuwa yeye alifanikiwa maishani mwake kwa jasho lake bila ya mwanaume yoyote kumsaidia.

Snura alieleza alivyotaabika alipotoka kwa wazazi wake na kuanza maisha ya kujitegemea, alisema kuwa ashawai lala njaa akiwa katika harakati ya kutafuta.

“Nilishalala njaa sana tu, tena wakati natoka kwa wazazi na kuanza maisha yangu binafsi ya kujitegemea, nilikuwa na wakati mgumu sana nakumbuka nilikuwa nashindia ugali na mbilimbi na nilikuwa jeuri sana japo nilikuwa na shida zangu kwa sababu maisha hayo hayakufanya nimtegemee mwanaume” alisema Snura.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere