Nilishamwambia Wema Atakuja Kupata Mtoto- Chuchu Hansy

Muigizaji wa Bongo movie Chuchu Hansy ameonekana kumkingia kifua msanii mwenzake wa Bongo movie, Wema Sepetu kuhusu suala lake la kuzaa mtoto.

Kwa kipindi kirefu Wema amekuwa akiweka wazi hisia zake juu ya watoto na kusema kuwa anapenda kuwa na mtoto siku moja lakini pia ameweka wazi wakati mgumu ambao amekuwa akipata katika jitihada za kupata mtoto.

download latest music    

Kipindi cha nyuma Wema alishawahi kuweka wazi kuwa miaka ya nyuma alishawahi kutoa mimba ya aliyekuwa mpenzi wake kwa kipindi hiko msanii Marehemu Kanumba, lakini tangu aweke wazi taarifa hiyo amekuwa akisakamwa mtandaoni na maadui zake ambao kila siku akimposti mtoto basi watamsema kwa nini hazai na vitu vingine.

Sikh ya birthday ya mtoto wa Ray na Chuchu anayeitwa Jayden , Wema alimposti mtoto huyo kwenye ukurasa wake Instagram jambo lililozua balaa kwani mashabiki walimvamia na kuanza kumnanga na kumuita mgumba tasa na majina mengine.

Kitendo kile hakikukaa vizuri na Chichi ambaye kwenye mahojiano aliyofanya na Enews ya East Africa TV alifunguka yafuatayo:

Kusema kweli zile comments zilikuwa nyingi sana lakini nyingi zilikuwa ni za kumuumiza mtoto kawekwa pale badala ya kusema happy birthday Jaden mtu anamuandiki liukurasa kabaisa maneno ya kumuumiza sijui mgumba sijui tasa hayo nimaisha na ni kipindi tu wao sio Mungu kama walimsema Ray ni tasa lakini leo hii Mungu kawaonyesha kampa mtoto kwaiyo na Wema asubiri kwa sababu siyo tasa alishabeba mimba mara ya kwanza lakini nilishamwambia Wema wewe utakuja kupata mtoto lakini sio pale unapohitaji wewe pale Mungu atakapopenda upate”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.