Nilitegemea Kuwa Tajiri Kama Diamond:-Juma nature
Msanii Juma Nature anasema kuwa kuwa miaka ya nyuma aliyokuwa akifanya kazi na album zake zilivyokuwa zikifanya vizuri alitegemea kuwa kama ingekuwa ni wakati huu basi angekuwa amenufaika sana na kutajirika sana.
Juma Nature anasema kuwa na yeye sasa angekuwa ni moja ya wasanii wachache wenye mafanikio makubwa sana kama walivyo wakina Diamond lakini ndio muda nao ulishapita.
kwa uuzaji ule wa album kwakwelitulikuwa tunafunikwa funikwa tu wala hatukuwa tunanufaika sana kama sasa hivi na hatukupaswa kuwa hivi.
nilitegemea kwa kipindi kile sasa hivi na mimi ningekuwa hata nina tv zangu kama mnavyomuona Diamond sasa hivi na viwanda vikubwa vya kwangu mimi mwenyewe.
Juma nature anasema kuwa pamoja na kwamba kuna vitu wanamiliki sasa hivi lakini ni kutokana na kukomaa kwao kama wasanii wa zamani.