Nimejaribu Kumtumia Meseji Lakini Hajajibu, Nandy Aongelea Nia Yake Ya Kumuomba Msamaha Ray C

Mwanamuziki wa Bongo fleva mrembo Nandy ameongelea nia yake ya kutaka kumtafuta Ray C ili waweze kumaliza tofauti zao licha ya Ray C kumuwekea ugumu.

Mwanzoni mwa wiki hii Ray C hakumkopesha Nandy kwani alimjia juu kwa kitendo chake cha kuimba nyimbo zake bila ruhusa yake kwenye tamasha linaloendelea la fiesta. Ray C aliweka wazi kukerwa na kitendo hicho hasa kwa sababu yeye mwenye nyimbo hakualikwa kwenda kushiriki tamasha hilo.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo, Nandy amefunguka ya moyoni kuhusu ishu hiyo name meseji aliyomtumia Rayc lakini hajaijibu:

Kiufupi ni kwamba tu niliposti clip ya nyimbo ya Mez B ambayo amemshirikisha dada angu Ray C ambayo tuliimba mimi na Ben pol na tulifanya hivyo kwasababu ilikuwa ni season ya kukumbuka malegend wa bongo fleva kwaiyo haikua kwa nia mbaya sasa nilishangaa kwa nini alichukulia vibaya mimi kuimba ile nyimbo yake hadi kupelekea mashabiki zake kunitukana sana lakini sikuishia hapo niliandika kama kumuelewesha na kumtaka radhi kwenye Instagram pia nilimwandikia meseji ya kawaida private nikamuuliza kwa nini kaamua kunifanyia hivi? Na ni siku gani nilishawahi kukutana naye sikumsalimia? Nikamwambia mbona mi nilikusapoti kukutangazia nyimbo yako ilipotoka lakini hata asante hukutoa! Lakini nilikuja kugundua hata mwaka jana nilivyoimba nyimbo yake hakupenda ingawa alikuwepo kwenye mazoezi na hata mashairi mengine mwenyewe alinisaidia”.

Nandy alimalizia kwa kudai kuwa amemsamehe Ray C na atachukua ushauri wake wa kuimba nyimbo zake mwenyewe kwani hata fiesta kupata kazi ni kutokana na watu kuvutiwa na  nyimbo zake mwenyewe na siyo nyimbo za Ray C au msanii mwingine yeyote.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.