Nimeshangazwa na Mauzo Ya Albamu Yangu Ya Money Mondays

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri kwa hivi sasa mrembo Vanessa Mdee ‘Vee Money’ amefunguka na kuweka wazi kuwa mauzo ya albamu yake yanafanya vizuri sana.

Vanessa alitoa albamu yake ya ‘Money Mondays’ mapema mwezi uliopita na amekiri kuwa ameshangazwa na mauzo ya albamu hiyo na muitikio wa watu ambao ni mashabiki zake.

download latest music    

Vanessa alifunguka hayo kwenye Interview aliyofanya na Global Online Tv ambapo amekiri kuwa hayakuwa mategemeo yake hasa ukizingatia kutoa albamu sio kitu ambacho kimezoeleka:

Albamu yangu ina miezi miwili tangia itoke na kusema ukweli nimestaajabishwa na mapokezi watu wanadownload kwa kasi kubwa sana watu wamenunua nakala original Kupitia wakala wetu tunaendelea Kuitangaza lakini naona kuna kama muitikio fulani.

Nina furaha sana kwa sababu maisha yangu hayapo kama yalivyokuwepo mwaka jana kwani sahivi mimi ni msanii ambayr ninamiliki Albamu na ni sifa kubwa kwangu kwani sikutegemea muitikio huu na sapoti yao nashukuru sana Watanzania”.

Kwa muda mrefu wasanii wa Bongo fleva walikuwa hawatoi albamu kwa kuogopa kutopata maslahi lakini hivi sasa jambo la albamu limerudi mezani tena na wasanii Kama Vanessa, Chin Bees na Diamond wameshatoa albamu zao.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.