Nina Wivu Sana kwa Mume wangu Hasa Akitoka Bila Mimi :-Mke wa Babu Tale
Mke wa bosi wa Diamond Platinumz , Babu Tale amefunguka na kusema kuwa ana kuwa anaona wivu sana pale mume wake anapotoka nyumbani bila kuambatana nae tena hasa anapojua kabisa kuwa mtoko anaotoka sio wa kikazi zaidi.
Maneno hayo aliyaongea mwanadada huyo alipokuwa akihojiwa wikiend hii alipokuwa ameambatana na mume wake katika sherehe nyumbani kwa zamaradi huko Bunju jijini Dar, ambapo mwandishi laimuuliza kuwa je mwanadada huyo huwa anajisikiaje pale anapoona mume wake akiwa anapiga picha na warembo wengine na picha hzio zikawekwa katika mitandao ya kijamii.
mwanadada huyo alisema kuwa wivu unakuwepo lakini haweiz kuendekeza kitu hicho maana anajua atharibu kazi “wivu upo lakini ndo inategemea upo kwa kiwango gani, na ukiendekeza wivu unakwama”
Na hata Babu tale alipoulizwa kuhusu kuambatana na mke mkewe baadhi ya sehemu alisema kuwa siku hiyo aliambatana nae kwa sababu hiyo ni sherehe ya kifamilia na wala sio ya kikazi.