Ninai-miss Menejiment Yangu ya Zamani:-Enock Bella

Msanii kutoa kundi la Ya moto Band Enock Bella amefunguka na kuongelea kwa jinsi gani ambavyo anatamani sana menejimenti yake ya zamani ambayo ilikuwa ikiwamiliki wasanii wote wanne wa kundi la Ya Moto band kuendelea kuwaongoza na kuwa natamani sana kundi lao lingeendelea kufanya kazi pamoja kwa sababu wametoka mbali.

Enock Bella ambae kwa sasa ameachia ngoma yake mpya ya ngoja kidogo anasema kuwa pamoja na kuwa alikaaa kimya kwa muda mrefu  lakini anashukuru Mungu kwa sababu mashabiki zake wamempokea vizuri na ngoma yake inaonekana kufanya vizuri.

download latest music    

mapokezi ya wimbo wangu yamekuwa mazuri sana,mara ya kwanza nilijua sauti yangu ni ya kawaida sana kwaio nyimbo haitakuwa nzuri lakini kumbe sio.wengine walisema kuwa kwanini nipo kimya, labda nimekufa kimuziki au nilikuwa nabebwa sana na kundi , nilikuwa natembelea nyota lakini sio kweli.

kwa sasa nina fight mwenyewe wala sina uongozi kwa sababu wao wanaokuja na kufanya  kazi na mimi lakini wamekuwa wanashindwa makubaliano yenu, kwaio hakija mtu tukaelewana vizuri basi tutafanya kazi.

ninaimiss sana menejiment yangu ya zamani, ningependa sana ya moto band iendelee kuwepo kwa sababu imenifundisha vitu vingi, ndo imenitengeneza mimi, imenifanya niwe hapa niwe hapa.

Ya moto band ilikuwa ikifanya vizuri sana katika muziki lakini ndoto za vijana hawa wanne zilikuja kuvunjika baada ya kundi hili kusambaratika huku kukiwa na sababu zisizoeleweka

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.