Nini Ajutia Kuchanganya Mapenzi na Kazi

Msanii wa muziki wa Bongo fleva aliyewahi kufanya vyema amefunguka na kusema wazi kuwa sio vizuri kuchanganya mambo ya mapenzi na kazi kwani utapotea kimuziki.

Nini aliwahi kuwa kwenye mahusiano na ya kimapenzi na msanii mwenzake Ney wa Mitego ambaye pia alikuwa bosi Wake kwani alikuwa amesainiwa chini ya Label yake.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Enews cha EATV, Nini amesema wazi kuwa kuna madhara makubwa sana endapo Msanii wa kike atasimamiwa na Mpenzi Wake kwani inaweza ikasababisha Msanii huyo kupotea kwenye gemu.

Kuna madhara kwa mtoto wa kike kusimamiwa na mpenzi Wake kwani tumeona wasanii wengi wa hivyo wameishia kati na hawajafikia malengo yao kwaiyo kama inaweza ikaepukika ni vizuri zaidi lakini cha muhimu wa wasichana kujitambua na kutambua wanataka nini”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.