Ninogeshe ya Nandy Yamfunika Ommy Dimpoz
Msanii wa kike Nandy ambae anatamba na wimbo wake wa Ninogeshe amkalisha chini msanii mkongwe pia Ommy Dimpoz na wimbo wake wa Yanje ambao pia ulitoka siku chache zilizopita, nyimbo hizo ambazo zote zinaonekana kuwa zinazopendwa sana na watu tangu zimetoka zimekuwa zikibadilishana nafasi kwa muda mrefu na sasa nandy amemkalisha ommy kwa nafasi moja.
Siku chache za nyuma msanii ommy dimpoz alisema kuwa hawezi kuangaika kufanya kiki ya kitu chochite ili kuweza kuifanua nyimbo yake ifanye vizuri, zaidi sana anaamini kuwa nyimbo zake za mwanzo zilishamtengenezea jina kubwa la kuweza kutoa wimbo wowote ili kuweza kuhit.
Nandy anakuwa moja y wasanii wa kike wanaofanya vizuri sasa katika muziki na kuwakalisha kina dada wengine wengi kutokana na kipaji chake ambacho amekuwa akikitendea haki.