Nisha Akana Kuwa na Mahusiano ya Kimapenzi na Brown

Muigizaji wa Bongo movie anayetamba kwa hivi sasa na wimbo wake wa Bachela Nisha, amefunguka na kudai habari zilizotapakaa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa ana Mahusiano ya kimapenzi na Ex boyfriend wa Wolper sio za kweli.

Kwa wiki kadhaa sasa kumekuwa na tetesi zilizotapskaa Kwenye mitandao ya kijamii zinazosema Nisha amemuopoa Ex wa msanii mwenzake Wolper aitwaye Brown, hii ni baada ya video zao kuonekana mitandaoni wakibusisna.

download latest music    

Tetesi hizi za Mahusiano na Brown zimezua maneno mengi hasa kwa watu wakiwashutumu wasanii wa Bongo movie kupenda kupokezana mabwana au kupenda kuchukuliana wanaume hasa viben ten.

Kwenye Interview aliyofanya Nisha na FNL ya East Africa Tv amekataa kuwa na Mahusiano na Brown alidai ile yote ilikuwa ni kiki ya kazi tu lakini hajawahi kuwa mpenzi wake:

Kwanza kabisa sinaga historia ya kutembea na bwana wa rafiki yangu au asiwe rafiki yangu ila Bachela ndio jina la mchezo kwaiyo unaweza ukaona kabisa kuwa sina uhusiano wowote na Brown zaidi ya kazi”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.