Nisha Amkwapua Brown Ex Wa Wolper

Muigizaji wa Bongo movie Nisha bebe ameingia Kwenye headlines Kwenye mitandao ya kijamii kwa hivi sasa baada ya kupatwa na skendo ya kumkwapua ex wa staa wa Bongo movie Jacqueline Wolper aitwaye Brown.

Habari inayo trend hivi sasa kwenye social media ni hii ya Nisha kuangukia kwenye penzi la Ex boyfriend wa Wolper aitwaye Brown na inasemekana kuwa wapo kwenye penzi zito balaa.

download latest music    

Habari hizi zilishika kasi ya ajabu baada ya wawili hao kuonekana kwenye video na picha mbali mbali kwenye social media wakiwa wanashikana na kuonekana kabisa wakiwa kwenye mapenzi mazito sana.

Gumzo hilo lilianza baada ya Brown kuposti picha akiwa ameshikana mikono na mrembo bila kuonyesha sura yake lakini baada ya muda mfupi Nisha alionekana kaweka picha ile ikawa kama profile picha yake Kwenye ukurasa wake wa Instagram na baadae aliposti video akitomaswa Tomaswa kichwa na Brown.

Mpaka hivi sasa hakuna aliyethibisha kwa maneno kama kweli wapo Kwenye Mahusiano hasa ukizingatia Nisha ana urafiki na Jacqueline Wolper ambaye aliachana na Brown mwaka jana mwishoni baada ya kuwa Kwenye Mahusiano kwa mwaka mzima.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.