Nisipozaa Nitakufa Kwani? Lady Jay Dee Amtolea Povu Zito Shabiki Aliyemshauri Azae

Mwanamuziki mkongwe wa kike wa Bongo fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jay Dee’ amemjia juu na kumtolea povu zito shabiki wake aliyemuombea kwa Mungu azae mtoto.

Lady Jay Dee amekaa kwenye sanaa ya muziki kwa kipindi kirefu sana labda kuliko msanii yoyote wa kike lakini moja kati ya vitu mashabiki wake hupenda kujua kuhusu yeye ni maisha yake binafsi.

download latest music    

Baada ya kuwa kwenye ndoa na mtangazaji wa Clouds Fm, Gardner G Habash kwa miaka kumi Lady Jay Dee aliomba talaka na kuachana kwa sababu zisizojulikana lakini tangu aachane na Gadner Jay Dee amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki kutoka Nigeria anayejulikana kama Spicy Music.

Moja kati ya vitu ambavyo huongelewa sana kuhusu Lady Jay Dee na maisha yake binafsi ni suala la kuzaa mtoto ambapo kumekuwa na teyesi nyingi kuwa hana uwezo wa kuzaa huku tetesi hizi zikizaliwa kutokana na kukaa kwenye ndoa kwa miaka kumi na zaidi bila kupata mtoto na umri wake kusemekana kuwa umeenda, Ingawa mwenyewe hajawahi kuliongelea suala hilo hadharani.

Siku chache zilizopita moja wa shabiki wa Lady Jay Dee aliandika kwenye ukurasa wa Lady Jay Dee kuwa anamuombea azae mtoto na anampensa sana maneno yaliyoelekea kumkera Jay Dee kwani alimtolea povu zito Sana:

Hivi hayo maswala ya kupata mtoto yanahusikaje hapa kwa mfano? Hivi si mngeniacha nipumua mtoto amekuwa mtoto kwani nisipopata itakuwaje kwani kwa mfano? Natakiwa nife au? na hii posti inahusikaje na mtoto? Jifunzeni kuwaachia watu maisha yao binafsi aisee mnanichosha zaeni nyie mjaze dunia inatosha”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.