Nuh Mziwanda Adai Na Yeye Alichangia Kununua Mjengo Wa Shilole

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nuh Mziwanda ameibuka kuwa ana yeye pia aliweka mkono Kwenye kununua Mjengo mpya wa Shilole aliouanika Kwenye mitandao ya kijamii.

Ikiwa ni siku chache zimepita tangibly shilole aanikr Mjengo wenye thamani ya zaidi milioni 90 anaoujenga hivi sasa, aliyekuwa mpenzi wake Nuh Mziwanda amedai na yeye pia ana chake Kwenye Mjengo huo.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Wasafi Tv, Mziwanda amedai pamoja na kwamba alishiriki kununua Mjengo huo wakati wa Mahusiano yao lakini amesem hawezi akaomba arudishiwe pesa sababu hawapo wote:

Ni kweli ule mjengo tulinunua wote Wakati tupo pamoja, nakumbuka tulikuwa na hela tukaenda mpaka kule tukamalizana na yule jamaa yaani mishe mishe zote tulikuwa wote tunanunua nyumba na kukamilisha kila kitu”.

Lakini pia Mziwanda amedai hawezi kumdai SHilole Pesa zake alizochangia Kwenye ule mjengo sababu yeye ni mwanaume:

Hapana siwezi kwa sababu yule mtoto wa kike ujue alafu mimi nilikuwa mwanaume kama Baba sasa nikianza kudai nilichangia hiki na kile inakuwa haileti picha nzuri yule ni mtoto wa kike muache atunzwe”.

Baada ya kuweka wazi mjengo wake Shilole aliweka wazi amejenga nyumba ile kwa nguvu zake bil msaada wa mwanaume yoyote na kusema ile sio nyumba ya mume wake Uchebe bali amejenga kwa ajili ya watoto wake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.