Nuh Mziwanda- Sina Bifu na Diamond Ila Sina Ukaribu Naye Pia

Mwanamuziki wa Bongo fleva Nuh Mziwanda amefunguka na kudai jana bifu na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Nuh ambaye ameshafanya ngoma na Ali Kiba aliomshirikisha katika wimbo wake wa Jike Shupa amefunguka na kusema hata kama hajawahi kufanya ngoma na Diamond haimaanishi wana bifu.

download latest music    

Mziwanda alifunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na Dizzim Online pale alipotakiwa kujibu tetesi kama ana tatizo lolote na Diamond:

Mimi sina bifu na Msanii yoyote na wala sina bifu na Diamond wala sina ugomvi naye unajua yule mchizi sana na tulishawahi kufanya vitu vingi sana lakini muda nakumbuka Times hafanyi shoo zake tulikutana Dodoma tukafanya shoo yake kwaiyo ni mtu ambaye yuko Poa lakini hatuna mawasiliano wala ukaribu wowote.

Lakini pia Mziwanda ameweka wazi kuwa kama ikitokea nafasi ya kufanya kazi na Diamond basi atafuata taratibu za kwenda Kwenye uongozi wake na kuomba Kolabo.

Kutokana na Bifu lililopo kati ya Diamond na Ali Kiba, wasanii wanaofanya kazi na wasanii hao hujikuta wakichagua upande wa kuwa na hivyo Mziwanda baada ya kufanya Kolabo na Ali Kiba alidaiwa kuwa na bifu na Diamond.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.