Nyota Ya Hamisa Mobeto Yazidi Kung’ara.
Pamoja na kwamba amekuwa akishambuliwa katika mitandao ya kijamii huku wengune wakumtuhumu vibaya hasa wale watu ambao ni mashabiki wa upande wake wa pili ,mwanadada Hamisa Mobeto amezidi kuonekana akiwa na nyota yenye kungaa baada ya kupata deal lingine alilosaini hivi karibuni.
Akionekana katika picha na moja ya mabosi wa kampuni fulani, mwanadada hamisa mobeto ameonekana mwenye furaha na mwenye kuonyesha sura ya mafanikio sana hasa baada ya kuweka picha hiyo akiwa tayari ameshasaini mkataba huo.
Hamisa ambae hivi karibuni alitoka kusaini mkataba mwingine wa kampuni ya Prima Afro anaendelea kuonyesha mafanikio yake hasa baada ya hivi karibuni kutoa wimbo wake na kuonyesha kupokelewa vizuri.