Nyumba Sio ya Hamisa, ni Nyumba ya Deedaylan;-Mama Mobeto
Mama mzazi wa mwanadada Hamisa Mobeto amefunguka na kusema kuwa Pamoja na kwamba ni kweli Diamond amemnunulia nyumba hamisa lakini nyumba hiyo sio ya hamisa kama watu walivyokuwa wakisema bali nyumba hiyo ni ya mtoto wao Abdul na amemshukuru sana mtoto huyo asie na mwaka hata mmoja kwa kuwafanya wakapewa nyumba.
Hamisa hajanunuliwa nyumba, kanunuliwa daylaan, huyu ndio mwenye nyumba na kwanza namshukuru mjukuu wangu kwa kuja katika maisha yetu.bila daylan tusingekuwa hapa
Hata hivyo Mama mobeto anasema kuwa anajua kuwa watu wanamchukia sana mtoto wake lakini waache na kwamba anajua kuwa ipo siku watakuja kumpenda kwa sababu swala la mwanaume kumchagua mwanamke wa kuona ilo ni swala la Diamond kuamua.
Najua kuwa mwanangu wanamchukia lakini ipo siku watampenda tu , naomba wamuache mwanangu wasimsakame wamuache swala la kuoa anajua kuchagua ni mwanaume.