Odama Apata Kigugumizi Tetesi Za Ujauzito.

Kumekuwa na tetesi za muda mrefu kuhusu msanii wa bongo movie Tanzania kuwa ni mjamzito  na kwamba aamekuwa akificha jambo hilo,hata hivyo msanii huyo alipoulizwa kuhusu swala hilo alijikuta akipatwa na kigugumizi na kushindwa kutoa tamko rasmi kuhusu swala hilo la yeye kuwa mjamzito .

Akiongea na star mix ya GPL,Odama kwa njia ya simu alisema kuwa kuhusu swala la yeye kuwa mjamzito ni swala nyeti sana,  hawezi kuongelea swala hilo kwa sababu yuko mbali na nyumbani.Hata hivyo alimuomba mwandishi kuwa mvumilivu mpaka atakaporudi ndio waweze kuzungumzia swala hilo.

download latest music    

.  Nipe muda  nilitafakari  swali lako, lakini  kama hutojali  tunaweza kuzungumza  mambo mengi  hilo naomba tuachane kabisa aidha unaweza kuningoja mpaka nirudi tuzungumze ana kwa ana kuhusu swala hilo  kwa sasa wala hata siwezi kukwambia kama nina mimba au sina. -Alisema Odama kwa njia ya simu.

Wasanii wengi wa kike wamekuwa wakishindwa kusema mbele za watu au katika vyombo vya habari kuhusu swala la wao kuwa wajawazito ingawa kuwa mjamzito ni swala la kheri kwa kila mtu

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.