Ommy Ahaidi Kuoa Tanzania, Asema Hatoki nje Kama Wengine.

Ommy dimpoz ambae hana siku nyingi tangu amewasili kutoa Afrika ya Kusini ambapo alikuwa akipatiwa matibabu ya maradhi yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu sasa amefunguka na kusema kuwa hana mpango wa kuoa nje ya nchi kama wanavyofanya wasanii wengine.

Akijibu maneno ya waandishi wa habari, amefunguka na kusema kuwa ingawa amekuwa na mpango wa kuoa wanawake wanne, anategemea kuwa kuwa watatu wote wanatoka tanzania na kama kuna mmoja ataongezeka basi anaweza kutafuta kutoka nje.

download latest music    

Kumekuwa na malalamiko sana kuwa wasanii wengi wa Tanzania wa kiume wamekuwa wakienda kuoa nje ya nchi na kuacha wanawake wa tanzania wakilalamikia swala hilo.

Ninawaahidi dada zangu wa Tanzania kuwa nitaoa Tanzania, watatu tanzania na pengine mmoja kutoka nje , maana naona wenzangu wote wanatoka nje.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.