Ommy Dimpoz Afunguka Jinsi Ugonjwa Wake Ulivyomuunganisha na Diamond

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz amefunguka na kueleza jinsi ugonjwa wake ulivyomrudisha na watu ambao aligombana nao.

Ommy Dimpoz amedai pamoja na kuumwa na Kupitia kipindi kigumu lakini anaamini ugonjwa wake umekuwa kama ibada kwani amejikuta akipata maombi ya watu wengi.

download latest music    

Sio siri kuwa Ommy Dimpoz na msanii mwenzake Diamond Platnumz walikuwa maadui kwa muda mrefu lakini siku chache zilizopita tulishuhudia jinsi Diamond alivyoweka tofauti zao pembeni na kumuombea kheri katika maradhi yake.

Kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv, Ommy Dimpoz amefunguka

Kuumwa kwangu naweza kusema imekuwa kama ibada unaweza ukajikuta hata watu ambao ulikuwa huongei nao wamekutumia meseji ya pole labda kutokana na kuguswa kwaiyo nimefarijika sana sana kwaiyo Nana huku tu Mungu kwa hapa nilipofikia”.

Lakini pia Ommy Dimpoz alifunguka kuhusu salamu za rambi rambi alizotumiwa na Diamond:

Kusema kweli sijawasiliana na Diamond mpaka hivi sasa lakini pamoja na kuwa wote Watanzania sisi pia ni ndugu kwaiyo amefanya jambo jema kunipa pole kwa sababu mimi ni mgonjwa na ndio ubinadamu zaidi”.

Lakini pamoja na kuonekana Diamond kuweka tofauti zake na Ommy na kumtumia salamu za pole Lakini pia aliyekuwa Meneja wake Mobenga ambaye pia hakuwa katika maelewano ameonekana kuweka tofauti zao pembeni na kwenda kumtembelea Ommy hospitali South Africa mara mbili tangu ameanza kuumwa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.