Ommy Dimpoz Afunguka Kuhusu Bifu Lake na Diamond

Staa wa muziki anayefanya vizuri kwa hivi sasa na kibao chake cha ‘Yanje’ Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz amefunguka kuhusu bifu lake na msanii mwenzake Diamond Platnumz.

Ommy Dimpoz na Diamond walikuwa marafiki kwa muda mrefu na hata kutoa pamoja nyimbo kali kama Prokoto na nyinginezo.

download latest music    

Lakini wasanii hao waliingia katika bifu zito miaka michache iliyopita hadi kupelekea wawili hao kupelekana polisi baada ya Ommy Dimpoz kumuongelea mama Diamond Mtandaoni.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Citizen Radio hivi karibuni Kwenye Media your nchini Kenya Ommy Dimpoz alipoulizwa kama bifu lake na Diamond litaishia alifunguka:

Kila jambo lina wakati wake kwa hiyo time itakapofika mambo yote yatakaa sawa, tuombe Mungu”.

Lakini pia Kutokana na mgawanyiko uliopo kati ya WCB na Team Kiba, Ommy Dimpoz aliulizwa endapo kuna nyimbo zozote anazozipenda kutoka kwa WCB:

Moja wapo ni hiyo kama unavyosema Kwa Ngwaru ni wimbo ambao unafanya vizuri, yeah!, kuna mwingine nimesikia wa Rayvanny Pochi Nene, kwa hiyo kwa currently ni nyimbo ambazo naweza kusema zinafanya vizuri“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.