Ommy Dimpoz Aweka wazi Chanzo cha Ugonjwa Wake ni Sumu.

kwa muda sasa msanii wa muziki wa bongo fleva amekuwa akiumwa na hata hivi karibuni kulizuka kwa maneno katika mitandao ya kijamii kuwa msanii huyo amepelekwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi zaidi yaani ICU .lakini baada ya kufatilia sana na watu wake wa karibu walikanusha msanii huyo kuwa ICU lakini walisema kuwa bado ni mgonjwa.

Baada ya kusambaa kwa taarifa hizo baadhi ya waandishi wakubwa nchi, Milladr ayo aliamua kumtafuta na kumjulia hali Ommy dimpoz na kutaka kujua hali yake na chanzo cha ugonjwa wake na ndipo alipifunguka na kusema :-

download latest music    

ugonjwa huu kwenye mfumo wangu wa chakula ulianza muda mrefu kidogo,nilikuwa nikiangaika katika hospitali tofauti Tanzania na kila nilipoenda walikuwa wakinipa majibu tofauti pia.wengi waliniambia kuwa koo langu linauvimbe na kwamba hii inasababisha kutoweza kupitisha chakula vizuri, wengine waliniambia nina kansa ya koo.

nakumbuka katika harusi ya alikiba nilikutana na Gavana Joh wa mombasa na akanisaidia kunikutanisha na madaktari nchini kenya, madakatari nchini kenya waliniambia kuwa ugonjwa wangu ulisababishwa na kunywa kitu chenye sumu na wakasema kwa ukubwa wa tatizo nililokuwa nalo inabidi kutibiwa nje ya nchi.

Hata hivyo Ommy anasema kuwa anaendelea vizuri na bado yupo huko kwa matibabu lakini hali yake inazidi kuimarika sio kama siku za nyuma.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.