Papii Atamani Kupanda Mwendokasi, Ashangazwa na Uwepo wa Mitandao ya Kijamii.

Ni miaka 14 tangu walipopata hukumu yao na kukaa gerezani kwa muda wote huo, kipindi hicho hakukuwa na mambo mengi ambayo wameyakuta sasa hivi yanaendelea katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia .Akiongea na Leo Tena ya Cloud Radio, Papii Kocha amefunguka na kuelezea mshangao wake aliokuwa nao baada ya kutoka gerezani baada ya kukaa muda wote huo.Katika vitu alivyokuwa akishangaa ni   uwepo wa mabasi ya  mwendokasi.

Nilipotoka jela nimeona vitu vingi sana vimebadilika, nimeshangaa sana kuona mabasi ya mwendokasi ila sijayapanda ila natamani sana kuyapanda , ninaogopa watu tu watakuwa wengi na maswali yatakuwa mengi.

Akiendelea kuelezea kuhusu vitu vingi alivyovikuta amesema pia  anasema kuwa mwaka 2003 wakati wanahukumiwa hakukuwa na mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter, whatsaap  na instagram lakini sasa hivi ametoka ameikuta ingawa hawezi kuitumia kunawatu wamekuwa wakimsaidia lakini ni mizuri.

download latest music    

Kweli hakukuwa na mitandao ya kijamii , tulikuwa tunatumia simu zile kubwa za twanga pepeta lakini kwa sasa kutumia hii mitandao ndugu zangu ndo wananisaidia nimeipenda mitandao ni mizuri sana.kuna mtu ananisaidia kutumia lakini whatsapp natumia mwenyewe.

Papii Kocha anasema kuwa mambo mengi yamebadilika sana hata kasi ya maendeleo ni kubwa sana kulinganisha na walivyokuwa wameacha na hata baadhi ya maeneo yamekuwa kama nje ya nchi .

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.