Papii Kocha Atangaza Kurudi Bendi Yake Ya Ngwasuma

Msanii wa muziki wa Dansi nchini Johnson Nguza Viking ‘Papii Kocha’ amefunguka na kuweka wazi kuwa ana mpango wa kurudi katika bendi yake ya Ngwasuma.

Papii Kocha ametangaza kujiunga na Bendi ya FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’ aliyokuwa akiitumikia kabla ya kupatwa na majanga ya kifungo cha maisha na baadaye kupata msamaha wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Papii Kocha alisema kuwa hafikirii kujiunga na bendi nyingine yoyote zaidi ya kurudi kwenye bendi yake hiyo ya zamani kwani bado anaipenda.

Kwa sasa nafanya kazi ya muziki kwenye maonesho mbalimbali nikiwa na baba (Babu Seya) kama wasanii binafsi lakini nikishatulia vizuri natarajia kurudi FM Academia na sifikirii kujiunga na bendi nyingine tofauti na hiyo“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.