Papii Kocha na Babu Seya Kupiga Bonge la Show ‘Vikings Night’

Wasanii wakongwe wa muziki wa Bongo fleva waliowahi kutamba na kibao chao cha ‘Seya’ Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Papii Kocha wanampango wa kufanya bonge moja la show itakayoitwa ‘The Vikings Night’.

Wasanii hao Baba na mwana waliokuwa jela kwa miaka zaidi ya 10 kwa mashtaka ya kubaka, ambapo walifanikiwa kuonja ladha ya uraiani mapema mwaka jana siku ya uhuru 9 disemba ambapo walitoka jela kwa msamaha wa raisi.

download latest music    

Tangu warudi uraiani miezi mitatu iliyopita wasanii hawa wanatarajiwa kufanya Show yao kubwa ya kwanza baada ya kuachiwa huru ingawa wameshafanya shoo chache hasa visiwani Zanzibar shoo hii inatarajiwa kuwa kubwa zaidi.

Shoo hiyo inatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi tarehe 10 machi katika ukumbi wa King Solomon Hall. Papii Kocha ameshatoa wimbo wake mpya unaoenda kwa jina la Waambie ambao Mpaka sasa tayari unafanya vizuri sana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.