Penny.Kupitia Lulu Tujifumze Kitu Katika Mapenzi

Vj Penny ni mmoja  wa wanadada warembo na wastaarabu katika tasnia ya sanaa, ambae kuna kipindi jina lake lilikuwa maarufu sana kutokana na kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msanii mkubwa Tanzania anaejulikana kama Diamond Platinumz.Mwanadada huyo ambae kwa sasa anafanya kazi nzuri ya kutangaza kipindi cha harusi yetu kinachorusha na televisheni za maisha Magic Swahili amefunguka na kuongelea hisia zake kutokana na kesi ya Lulu na hukumu yake kwa ujumla.

Akizungumza na Global Vj Penny amesema kuwa watu wanapaswa kujifunza kitu kutokana na yale yaliyompata Lulu Michael na sio kukaaa na kuanza kumsimanga au kumsema vibaya kwa sababu kila mtu anapitia katika mambo ya mapenzi na ni vigumu kujua lipi litakutokea litakalokufanya uende alikoenda lulu.

download latest music    

jamani kwa kweli hakuna hata haja ya kumsema lulu vibaya, au kumcheka kwa sababu matukio kama hayo yanaweza kumpata mtu yoyote na wakatui wowote ule, na pale mwenzio anapopata jambo kama ilo ni vizuri zaidi kumuombea. -Alifunguka Mwanadada huyo.

Lulu amabe alipata hukumu yake ya kuua bila kukusudia tarehe 13 November alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerzani kama adhabu baada ya kumuua msanii wa bongo movies marehemu Steven Kanumba miaka mitano iliyopita ambapo wawili hao walikuwa na uhusiano wa kimapenzi wa kisiri siri.

Hata hivyo baada ya hukumu ya lulu ni mambo mengi yamesemwa katikamitandao ya kijamii na wa watu maarufu na mashabiki pia ambapo wapo waliokuwa wakimuhukumu vibaya na pia wapo waliokuwa wakimuombea meme msanii huyo.

Vj Penny ni moja wa watu maarufu wa kike tanzania wasiokuwa na skendo katika mitandao, na yeye baada ya kugombana na Diamond Platinumz hakuwahi kuwa kama wasichana wengine ambao wamekuwa kutwa wakijianika katika mitandao ya kijamii wakitaka kujulikana.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.