Penzi La Lulu Diva na Kigogo Aliyekuwa Anamuweka Mjini Lafika Mwisho

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri sana Lulu Abbas maarufu kama Lulu Diva anadaiwa kumwagana na Kigogo aliyekuwa Ananias heuristic hapa Mjini.

Global Publishers wanaripoti kuwa kigogo huyo alimwagana na Lulu Diva hivi karibuni japokuwa mwanadada huyo amekuwa akifanya kuwa ni siri kwani anahofia watu ‘watamzodoa’ kwa maneno endapo wakiujua ukweli.

download latest music    

Yule kigogo aliyekuwa anampa jeuri Lulu Diva amemmwaga na amemnyang’anya mpaka lile gari la kifahari alilokuwa anajidai nalo mjini, sasa sijui itakuwaje na ataishi vipi maana ameshazoea kujishaua nalo”.

Baada ya Tetesi hizo, Gazeti la Amani lilimsaka Lulu ili kupata ukweli wa taarifa hizo ambapo aliweka wazi kuwa hajaachwa na Kigogo huyo bali wameachana na sababu kubwa ni mwanaume huyo kukosa uaminifu.

Yaani unajua kuna kipindi kingine mwanamke unapaswa kujifunza kujiongeza mwenyewe ndiyo moja ya mafanikio yako. “Siyo kila wakati umtegemee mtu akuongoze kwenye maisha yako kitu ambacho kimepitwa na wakati na ndiyo maana nikaamua kuendelea na maisha yangu na kupiga kazi tu“.

Lakini pia Lulu Diva amekana vikali tetesi za kunyang’anywa gari na nyumba baada ya Penzi kuisha.

Gari bado ninalo, kuhusu nyumba si ndiyo unaona bado ninaishi hapahapa jamani? Nitaendelea kukaa hapa maana nina uwezo wa kulipa kodi kupitia muziki wangu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.