Peter Msechu Adaiwa Kuachwa na Mchumba Wake

Mwanamuziki wa Bongo fleva Peter Msechu aliyetamba na wimbo wake wa ‘ Nyota’ na Malava amekumbwa na kashfa nzito ya kuachwa na mchumba wake na mama wa watoto wake.

Kwa habari za kimbea zilizo chini ya kapeti zimedai kuwa mwanamke huyo ambaye Peter Msechu amekuwa naye kwa miaka mingi na kumvalisha pete ya uchumba miaka mitatu iliyopita amemuacha huku sababu zikipingana kwani kuna waliodai ameachwa kwa sababu ya uzito mkubwa na wengine wanadai chanzo ni wadhfa.

download latest music    

Baada ya tetesi kutembea kwa muda kidogo Peter Msechu amefungukia tuhuma hizo kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha XXL ya Clouds Fm ambapo amesema haya;

Hayo ni mambo yangu binafsi ya kifamilia yaachwe yamalizike kifamilia mengi yanasemwa sana lakini mimi mwenyewe nitasema muda muafaka ukifika na pia naomba watu wasitunge tu vitu vyao wasubiri wasikie tamko kutoka kwa muhusika ambaye ni mimi ila familia yangu ipo Salama kabisa kama kuna la kusema basi nitasema ila kwa sasa tuache tu na mimi namuachia Mungu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.