Peter Msechu Akana Tetesi Za Kufulia Kimuziki

Msanii wa muziki wa Bongo fleva aliyewahi kutamba na ngoma zake kama vile Relax na Nyota amekataa tetesi ambazo zineku a zikisemwa juu yake kuwa amefulia.

Tetesi za Peter Msechu kufulia zilitokana na ukimya wake Kwenye gemu kwa kipindi kirefu bila ya kuwa na nyimbo iliyofanya vizuri kwa muda mrefu kama ilivyokuwa siku za nyuma.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Peter Msechu amesema kwa sasa anaimarisha shughuli zake za ujasiriamali ambazo zinamuingizia kipato kikubwa cha kuandaa sherehe, kupamba maharusi na shughuli mbalimbali za kijamii.

Ninawezaje kufulia kimuziki? Kwa watu wanaonifuatilia wataona pia nimefanya kava ya Wimbo wa Sitabaki Nilivyo. Hiyo inaonyesha kwamba bado nipo na uwezo wangu ni mkubwa. Ila nimeamua kidogo kuimarisha kwanza masuala yangu ya ujasiriamali tu“.

Peter Msechu ameweka wazi kuwa kwa sasa anafanya muziki jitihada zake amezielekeza Kwenye biashara zake zitakazoweza kumuingizia kipato kikubwa kitakachoweza kumkwamua kimaisha.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.