Petit Man Afungukia Kuvunjika Kwa Ndoa Yake na Esma

Mdau wa Sanaa ya Bongo fleva ambaye pia anasimamia wasanii wenye majina makubwa kama vile Country Boy, Petit Man wakuache ameibuka na kuongelea Ndoa Yake na Esma.

Petit Man aliyekuwa  kwenye ndoa na Dada wa staa wa Bongo fleva nchini Diamond Platnumz aitwaye  Esma Platnumz amefunguka kuhusu kuvunjika kwa Ndoa hiyo.

download latest music    

Baada ya kuishi kwenye ndoa kwa miaka minne na kufanikiwa kuzaa Mtoto mmoja ajulikanaye kama Taraj wawili hao walisemekana kuachana mapema mwaka huu.

Kwenye mitandao ya kijamii kuna skendo ilisambaa kuwa Petit hakuwa mwaminifu kwa mke wake hadi kupelekea kuzaa na mwanamke mwingine kipindi cha ndoa yao.

Katika mahojiano aliyofanya na Millard Ayo, Petit Man kwa mara ya kwanza ameweka wazi suala la kuachana Man Esma:

Kwenye mahusiano kuna makosa, kila Binadamu ameumbwa lakini ana mapungufu yake, Mimi na Esma tuliishi miaka mitano siwezi weka hadharani yaliyotokea yule ni Mke wangu tumezaa nae, matatizo yapo ni kawaida” .

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.