Petit Man: Bill Nas Sipo Naye Tena

Petit Man Wakuache anayejulikana kwa ukaribu na kufanya kazi na mwanadada Wema Sepetu amefunguka kuhusu kuacha kumsimamia mwanamuziki wa Bongo fleva Bill Nas anayefanya vizuri na ngoma yake ya Sina jambo.

Petit Man alikuwa anawasimamia Bill Nas na Country Boy kupitia kampuni yake ya usimamizi/ management company inayoitwa ‘Living Fast Living Good’ (LFLG).

download latest music    

Petit Mama amevunja ukimya na kudai kuwa ameamua kujitoa LFLG na sababu ya kujitoa kwenye kundi hilo ni kuwa amedai anataka kuanzisha kundi/ label yake binafsi licha ya watu kudai kuwa Petit man na Bill Nas walichana kwa uhasama Mkubwa.

Inasemekana kuwa Petit ameondoka LFLG kwa sababu ya ugomvi uliotokea na kutokana na kwamba LFLG kulikuwa na mameneja wawili yeye Petit na Mchafu hivyo alivyoondoka aliosepa na Country boy na Mchafu akabaki na Bill Nas.

Kwenye interview aliyofanya na Enews ya East Africa TV Petit amefunguka haya kuhusu sababu za kutengana na msanii wake Bill Nas:

Mimi nimejiengua LFLG sipo tena LFLG panini sio kwamba nimejitoa kwa matatizo au kwa ubaya na ugomvi hapana ile itabaki kuwa ni familia yangu na mchafu ni braza wangu na pia Bill Nas bado mshikaji wangu kiroho safi kabisa maskani kama kawaida panini sahivi niko na Rooftop ambao nimeingia nao share ambapo nawasimamia baadhi ya wasanii akiwemo Country Boy”.

Lakini pia Petit amekiri kuwa pamoja na kwamba Bill Nas ni msanii mzuri na amefanya naye kazi kwa zaidi ya miaka mine lqkini anaamini ulifika wakati wa kila mtu kwenda upande wake ingawa hawana ugomvi na bado anamsapoti kwenye kazi zake.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.