Petit Man Hajahusika Kufuta Video Yangu Youtube- Billnas

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayetamba kwa miondoko yake ya kurap Billnas ameibuka na kumkingia kifua Petit Man Wakauache na kusema hajahusika katika kufuta video yake Youtube.

Kwa muda mrefu Petit Man alikuwa anasimamia kazi za Billnas mpaka pale alipohiondoa Kwenye Label hiyo mwaka jana mwishoni hivyo kuacha kumsimamia Billnas.

download latest music    

Siku ya juzi Billnas alilalamika kufutwa kwa video yake mpya ya wimbo wake ‘LAbda’ na watu wasio julikana na mara moja tetesi zilianza kutembea na Petit alinyoshewa vidole na kudaiwa kuhusika.

Lakini Kwenye Interview na kituo kimoja cha habari Billnas amemkingia kifua Petit Man na kudai sio yeye Lakini pia amesema sio mara ya kwanza anafanyiwa mchezo huo mchafu:

Sio mara ya kwanza watu kutoa video Yangu Youtube na sielewi kwanini wananifanyia hvyo maana mimi aio mtu wa kupiga views milioni 10, sijajua ni nani anafanya hivyo lakini sio Petit Man kama watu wanavyodai.

Naamini mtu anayenifanyia hivyo anataka kunikwamisha maana hakuna kingine anachofaidi akishanifanyia mimi hivyo”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.