Picha Ya Uchi Ya Faiza Imemponza Polisi Wameingilia Kati

Mwanamitindo na muigizaji wa Bongo movie Faiza Ally amejikuta katika wakati mgumu baada ya picha aliyoweka mtandaoni akiwa uchi anamzaa mtoto wake kumuweka matatani na jeshi la polisi.

Wikiendi iliyopita Faiza alitawala headlines zote baada ya kuamua kuweka mtandaoni picha iliyomuonyesha akiwa uchi leba anazaa. Watu wengi walishangazwa na kujiuliza kuwa ni kwanini Faiza aliamua kufanya kitendo cha fedheha kiasi kile huku wanawake wengi hadi  mastaa kama Snura walimuomba acute kwani anawadhalilisha wanawake wenzie lakini Faiza kuonyesha kuwa hajali alisema baadae angerusha video kabisa inayomuonyesha wakati anazaa.

download latest music    

Hii siyo mara ya kwanza kwa Faiza kufanya vitendo kama hivi kwani alijipatia umaarufu kwa kuweka picha za uchi au picha zinazomuonyesha akiwa amevaa nusu uchi mtandaoni.

Baada ya kuenea kwa kasi kwa picha hiyo siku ya jana kupitia ukurasa wake wa Instagram Faiza aliwaeleza mashabiki zake kuwa namba yake haitakuwa ikipatikana kwa muda kwani polisi wamezichukua kwa uchunguzi zaidi:

Wateja wangu Simu yangu itakuwa haipatikani kwa muda kwani polisi wamezichukua na sijui watakaa nazo kwa muda gani kwa iyo mliotuma pesa zenu kwa ajili ya mzigo msijali ziko katika mikono Salama na mizigo yenu itafika kwa wakati”.

Baada ya hapo baba watoto wa Faiza aliweka wazi kuwa yeye ndio anatuma taarifa katika mitandao ya kijamii kwani Faiza hayupo. Mpaka sasa hawajaweka wazi ni mini Faiza ameambiwa na polisi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.