Pretty Kind Afurahia Kuvunjika Kwa Penzi La Mobetto na Diamond

Video vixen na Msanii wa Bongo fleva Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind ameibuka na kuchekelea kuvunjika kwa mahusiano kati ya staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na Hamisa Mobetto.

Wiki chache zilizopita Mobetto aliweka wazi kuwa baada ya miaka kumi ya kuwa pamoja na Diamond na kuzaa mtoto mmoja wameachana rasmi na kila mmoja kuendelea na maisha yake.

download latest music    

Baada ya taarifa hizo za kuachana kwa Mobetto na Diamond Pretty Kind ameibuka na kudai amefurahishwa na Taarifa hizo kwa sababu yaliyotokea ni Mungu kaamua kumuumbua Mobeto kutokana na uchawi aliokuwa anamfanyia Diamond na hilo ni fundisho kwa wasichana wengi wanaoamini uchawi katika mapenzi.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Pretty Kind ametiririkia haya:

Kilichomtokea Mobeto ni fundisho kwa wasichana wengi na wanatakiwa kujua kwamba mapenzi hayalazimishwi na kamwe uchawi hauna nguvu katika mapenzi”.

Lakini pia Pretty Kind asihangaike sana kutangaza kuwa ameachana na Diamond huku akiwa bado anamuhitaji pia ajue kwamba hawezi kuolewa na msanii huyo bali yupo mke wa Diamond atakayeolewa hivi karibuni kwake yeye haiwezi kutokea.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.